Tuesday, 15 November 2016

GROUNDING(EARTHING) NI NINI?



Kwa kawaida kama ilivyo kwa binadamu, umeme unataka kupita katika njia fupi na rahisi kupitika. Umeme hupita katika njia iliyo rahisi kwake kurudi ardhini. Njia pekee inayotumiwa na umeme kurudi ardhini bila madhara yote ni kupitia katika waya ambao kwa lugha ya kiingereza unaitwa Earth Wire na kisha Earth Rod.  Mchakato mzima wa kukamilisha ufanyaji kazi wa huu mfumo unaitwa Grounding. Ikiwa kutatokea tatizo katika waya unaobeba umeme baada ya matumizi(neutral wire), au tatizo lolote la kiufundi ambalo litasababisha ongezeko la ghafla la umeme kutokana na radi kwa mfano, basi earth wire itaubeba umeme huu wa ziada kwenda ardhini. Kwa muunganiko huu wa earth wire na earth rod, ardhi inafikika kirahisi sana na umeme. Maana yake ni kwamba mfumo huu wa grounding una wajibu wa kumlinda mtumiaji wa umeme inapotokea tatizo la umeme.

Ikiwa radi ingepiga katika nyumba yako ingeweza kusababisha hatari katika mfumo wako wa umeme na madhara mengine(Soma kuhusu radi katika somo lililotangulia). Lakini kama mfumo huo umeunganishwa ipasavyo na mfumo wa earth(Grounding) kiasi chote cha umeme wenye madhara kwa mtumiaji au vifaa vya umeme kitaishia ardhini badala ya kuunguza kila kitu kilichounganishwa katika umeme kwa wakati huo au kumdhuru binadamu.

Sote tunafahamu kwamba ardhi ni kipitisha umeme kizuri kwa asili yake. Na kama nilivyosema awali umeme unapenda kupita katika njia rahisi na fupi, kwa hivyo ku-ground mfumo wako wa umeme ni kuufanya umeme wenye madhara kwako kupata mahali pa kupita kwa urahisi badala ya kwenda ardhini kupitia mwili wako. Hivyo kwa kifupi kabisa, Earthing au Grounding ni kuunganisha vifaa vyako vinavyotumia umeme katika ardhi ya dunia kwa kutumia waya(Earth wire) na fimbo(Earth rod) mara nyingi ya shaba ambayo huzikwa katika ardhi yenye unyevu wa kutosha.
Previous Post
Next Post

About Author

2 comments: