Wednesday, 9 November 2016

MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA UNAPONUNUA BULB KWA MATUMIZI YA NYUMBANI




Katika hali ya kawaida kabisa sitegemei mtu atamtafuta fundi umeme inapotokea taa imeungua katika chumba, ofisi au nyumba yake. Kwa yeyote yule, taa isipowaka jambo la kwanza atakalofikiri ni taa kuungua. Mara nyingi ukweli huwa ni huo isipokuwa labda kama imetokea ni idadi fulani ya taa haziwaki na kwamba tatizo hili limeanza kwa muda mmoja basi huwa kuna sababu zingine za kiufundi. Nataka kutoa ushauri kwako kuhusu mambo muhimu ya kuzingatia unapoamua kununua bulb mpya.

Kutokana na ongezeko la aina tofauti tofauti ya taa zinazotumia umeme, ni ukweli kwamba kumetokea machaguo mengi ya kutosha ya taa hizi.  Ni vizuri ukazijua aina mbalimbali ya taa zinazotumia umeme kidogo. Pamoja na kuwepo aina nyingi sana ya bulb, leo ntaongelea aina mbili tu ambazo ndizo za kileo na zinatumia umeme kidogo kama ambavyo umeziona katika picha hapo juu mapema. Kuna Compact Fluorescent Light(CFL) ambazo wengi tumezoea kuziita Energy Savor na Light Emitting Diode(LED) ambazo kwa hapa Tanzania wengi huzitumia sana katika umeme wa mfumo jua (Solar Power) na kwenye Tochi nyingi sana za siku hizi.

Bulb za kawaida (Incandescent bulb) ambazo zilizoeleka kwa miaka mingi, kwa sasa wengi hawazitumii kabisa ingawa bado zinapatikana madukani. Imekubaliwa na wataalam duniani kwamba taa za ina hii zisitengenezwe tena ila zilizokuwa tayari zimetengenezwa ziuzwe mpaka pale zitakapoisha. Taa hizi zinapatikana katika ukubwa wa 100W, 80W, 60W na 40W. CFL na LED zinatumia umeme kidogo sana japo nazo zinazidiana. Hapa chini nakuonesha kiasi cha umeme kila aina ya taa inatumia kwa kiasi kile kile cha mwanga inachotoa.

Bulb ya kawaida            CFL(Energy Savor)              LED
         100W                              20W                            18W      
           60W                              12W                            10W
           40W                               9W                               6W


  1. Ijue aina ya bulb fitting unayotumia. Hapa namaanisha ujue aina ya mahali unapofunga au kuchomeka taa yako. Kuna bulb fitting za pin na screws yaani za kuchomeka taa au kuiweka kwa mtindo wa kuzungusha kwa maana ya kufunga. Kama huwezi kutofautisha aina hizi ni vizuri ukachukua taa iliyoungua na kwenda nayo katika duka unalotaka kununua.
  2. Kama nilivyosema awali, kuna aina nyingi ya bulb kwa sasa. Usiogope kununua Energy savor au LED kwa sababu ya ughali wa bei yake, kununua bulb za aina hii kutaokoa gharama kubwa sana kama nilivvoonesha tofauti ya matumizi yake ya umeme hapo juu. Faida kubwa zaidi ni kwamba taa hizi hudumu kwa muda mrefu sana ukilinganisha na hizi za kawaida.
  3. Tambua rangi na ukubwa wa mwanga unaohitaji. Maana yake ujue ni taa ya Watts(W) ngapi unaitaka, usinunue tu ili mradi umepata taa mpya. Mwanga unaohitaji utategemea na ukubwa wa chumba na matumizi ya chumba chenyewe. Kadri chumba kinavyokuwa kikubwa kitahitaji taa yenye mwanga mkubwa zaidi. Ni vzr ukajua pia kwamba kadri Watts zinavyoongezeka ndivyo  mwanga unakuwa mkubwa.
  4. Tafuta taa yenye umbo na muonekano mzuri. Wengi wanaweza kubeza hili, Ukweli ni kwamba kila aina ya umbo ina namna yake ya kusambaza umeme katika chumba. Angalia maumbo tofauti ya bulb niliyoonesha hapo juu. Hata hivyo muonekano mzuri wa bulb hupendezesha pale ilipo. Aina ya umbo hutegemea pia mahali kitanda kilipo kwa chumbani au mpangilio wa meza na viti sebuleni.
  5. Nunua taa yenye viwango unavyohitaji. Bulb iliyokidhi viwango itadumu kwa muda mrefu, hutoa mwanga wake haraka mara baada ya kuwashwa, haizalishi joto na haipotezi uwezo wake kutokana na kutumika kwa muda mrefu. Angalia taa itakayotumia umeme kidogo kutoa mwanga wa kutosha.
  6. Nunua taa kulingana na matumizi ya chumba au jengo. Ikiwa ni ghala huwezi kununua taa kama unayotumia sebuleni, au chooni ukanunua taa kama unayotumia chumbani. Huhitaji taa ya mwanga mkali chooni, bafuni au stoo. Ikiwa ni chumba cha kusomea bila shaka utahitaji taa yenye mwanga wa wastani ambao sio mdogo wala sio mkali sana. Ikiwa utakuwa katika mwanga unaoumiza macho yako ni vizuri ukaomba ushauri au ukabadilisha taa mwenyewe.


Previous Post
Next Post

About Author

1 comment:

  1. Ford ecosport titanium - titanium-arts.com
    Ford ecosport damascus titanium titanium. 1. The website is located in the northern part of the Republic nano titanium babyliss pro of Cancun. The titanium body armor website is located in the country titanium money clip of Curacao, titanium piercings which is

    ReplyDelete