Hapa jengo linajumuisha nyumba unamoishi, ofisi, duka,
ghala,nk. Kwa ujumla bila ukaguzi wa
mara kwa mara katika maeneo hayo niliyoyataja na mengine mengi kunahatarisha usalama
wetu. Wengi wetu hatujui ni lini au ni baada ya muda gani tangu majengo yetu
yawekwe umeme kwa mara ya kwanza tunahitaji kuyakagua tena. Kadri
utakavyoendelea kunifuatilia utafahamu polepole mambo yote haya na mengine
mengi kuhusu umeme.
Nitajitahidi kuelezea
kwa lugha rahisi sana ili kila mmoja wetu aelewe. Kuna sababu nyingi za kufanya
ukaguzi huu kila inapobidi, lakini sababu ya msingi sana ni usalama(Safety).
Dalili kubwa ya kwanza inayoonesha jengo halikufanyiwa ukaguzi (ukiachilia
mbali sababu zisizoepukika) ni pale linapotokea tatizo kubwa kama janga la moto
au mtu kupigwa na umeme(electrocution). Kufanya ukaguzi wa mara kwa mara
kunapunguza uwezekano wa majanga kama haya kutokea.
Ik
iwa wewe ni mwajiri,
ni kwamba chini ya sheria za afya na usalama sehemu ya kazi
(Occupational Health and Safety Act) unatakiwa kuweka mazingira salama ya
mahali pa kazi kwa waajiriwa wako. Hii ni pamoja na kufanya ukaguzi wa mifumo
ya umeme katika maeneo yako.

Baadhi ya vitu vinavyotakiwa kukaguliwa ni pamoja na vifaa
vyote vinavyotumia umeme, swichi za kuwashia taa, swichi za ukutani, swichi
kuu, waya zilizotumika, kikata umeme(circuit breaker), mfumo wa earth, n.k.
Kumbuka: Ili kufanya ukaguzi ulio makini na unaozingatia taalumaya umeme, fundi
atalazimika kuzima umeme katika jengo lako wakati fulani na atahitaji kuyafikia
maeneo yote ya nyumba yako(sio baadhi).
Ukaguzi wa mifumo ya umeme kutokana na mazingira yetu
unapaswa kufanyika;
Ø Wakati nyumba /jengo lina zaidi ya miaka
kumi(10) tangu lilipofungwa umeme kwa mara ya kwanza.
Ø Wakati unanunua nyumba/jengo jipya.
Ø Wakati umefanya ukarabati mkubwa katika
nyumba/jengo lako.
Ø Wakati unaongeza vifaa vingine vinavyotumia
umeme ambavyo awali havikuwepo.
Ø Wakati unagundua kwamba matatizo ya umeme
yanajirudia mara kwa mara katika nyumba/jengo lako.
Ø Au wakati unagundua kwamba matumizi ya umeme ni
makubwa(malipo ni makubwa) kuliko uhalisia.
Ø Na wakati mwingine kikata umeme(Circuit Breaker)
inapokuwa inakata umeme mara kwa mara.
Ikiwa una maswali au dukuduku lolote tumia email yangu kabukaasa@gmail.com nitajibu maswali yako.
Nitaendelea pia kukuletea mambo mengi ambayo
nimegundua wengi hawajui ingawa ni madogo madogo na muhimu kwao. Ni mambo
ambayo huhitaji kwenda darasani ila unahitaji ufafanuzi na maelezo kiasi kutoka kwa mtaalam. Kesho
ntakueleza namna ya kuchagua jokofu linalokufaa.
0 comments: