Friday, 14 April 2017

IJUE TOFAUTI KATI YA VOLTAGE, CURRENT NA RESISTANCE.

Walio wengi wamekuwa wakichanganya maana hasa ya voltage na current. Katika vifaa vingi vinavyotumia umeme majumbani mwetu ni kawaida kuona maelezo kadhaa. Kwa mfano utaona 220V, 50H, 2A, 100W, n.k. Haya ni maelezo muhimu unayopaswa kuyafahamu japo kwa kiasi kidogo.

Nchi ya kwetu inatumia umeme ulio katika kiwango cha 220V, inaweza kufikia 240V. Nchi zingine kama Marekani na zingine zinatumia umeme ulio katika kiwango cha 110V. Ni muhimu kujua mambo haya. Tukumbuke kwamba naongelea umeme ulio katika mfumo wa line moja (Single Phase  System), yaani waya mmoja wa live na ule wa neutral.

50Hz inaonesha frequency inayokubalika katika nchi yetu. Kwa nchi nyingine hasa zinazotumia 110V utagundua wa frequency yao ni 60Hz. Sina uhakika kama kuna maneno rasmi ya kiswahili kwa maneno haya Voltage na Current.
Resistance kwa kiswahili kisicho rasmi ni Ukinzani. Unaweza kutengeneza akilini mwako picha ya bomba linalopitisha maji yanayosukumwa na pampu ya maji. Ile Pressure ya maji ndio Voltage kwenye umeme, kile Kiasi cha Maji kwenye bomba ndio Current. Kwa kifupi kabisa nafikiri unaweza ukawa umepata picha ya maana rahisi ya voltage na current. Ukinzani ambao maji yanakutana nao wakati yakisukumwa ndani ya bomba ni sawa na Resistance katika umeme.

Kipimo cha current ni Ampere(A), voltage ni Volt(V) na resistance ni Ohm. Kwa uelewa zaidi angalia picha niliyoiambatisha na maelezo hayo.

Previous Post
Next Post

About Author

1 comment:

  1. Maelezo mazuri sana kwa mtu wa kawaida ambaye hajasoma Physics!

    ReplyDelete